Toure ambaye ni mshindi mara nne mfululizo wa tuzo ya mchezaji bora Afrika, alikuwa na matumaini ya kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya tano ila anashangazwa na shirikisho la soka barani Afrika kudharau mafanikio yake ya kutwaa taji la mataifa ya Afrika na kumpa tuzo Aubameyang, kwani anaamini Kombe hilo halithaminiki.
Pierre -Emerick Aubameyang akikabidhiwa tuzo na rais wa CAF
“Nimesikitishwa sana sana na jambo hili ni aibu kuona Afrika tunavyoichukulia, hatutoi kipaumbele kwa mashindano yetu ya ndani. Nafikiri tumeitia aibu Afrika. Tumeifanya Afrika isionekane muhimu mbele ya macho yetu, tunathamini mafanikio ya nje ya Afrika kuliko ndani ya bara letu”>>> Yaya Toure
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 ameongea hayo baada ya kufanya mahojiano na kituo cha radio cha RFI, nakueleza kushangazwa na ushindi wa Aubameyang katika tuzo hiyo na yeye kupotezewa, licha ya kuwa ametwaa taji la mataifa ya Afrika kama nahodha wa Ivory Coast.
0 comments:
Post a Comment