Wimbo wa SORRY wa CHRIS BROWN Waibua Maswali!

chris-brown 
NEW YORK, Marekani
WIMBO wa hivi karibuni alioutoa Mwanamuziki Rick Ross akimshirikisha Chris Brown unaokwenda kwa jina la Sorry, umeibua maswali kutokana na mashairi yake kuwagusa wapenzi wa zamani wa Chris, Karrueche Tran na Robyn Rihanna Fenty.
2777A37E00000578-3035195-Wanting_her_back_Chris_has_reportedly_been_trying_to_win_back_Ka-a-28_1428779582112 
Wadau baada ya kusikiliza wimbo huo wamebaki njia panda huku wakishindwa kuelewa wimbo huo ni maalum kwa nani kati ya wawili hao. Hata hivyo, wengi wanaamini Sorry ni kwa ajili ya Karrueche baada mshkaji huyo kubainika ana mtoto wa siri aliyezaa na mwanamke mwingine.
Wengine wanadai mashairi yaliyomo kwenye wimbo huo yanamgusa moja kwa moja Rihanna. Ndani ya Sorry, Chris amejaribu kuonesha majuto yake kwa kumuumiza mpenzi wake (hakumtaja) na kuahidi kuwa mwema kwa atakayempata baadaye.
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment