Q-Chief Kuwashirikisha TID na DIAMOND

Q-Chief amesema tayari amesharekodi wimbo wa pamoja na swahiba wake TID na sasa yupo kwenye mazungumzo na Diamond Platnumz kuhakikisha anaibariki pia ngoma hiyo.
Q amesema baada ya kuona wamemaliza tofauti zao, alimshauri TID kufanya wimbo wa pamoja kama wasanii wakongwe wa muziki wa Bongo Flava. “Nimerekodi na TID ambaye tulikuwa tuna mgogoro ndani ya miaka 6 au 7 na kila mtu anajua,” Q-Chief ameiambia Bongo5.
“Lakini tumemaliza tofauti zetu, sisi kama watu wazima tunajitambua na nikamwambia hebu tujaribu kufanya ngoma fulani kama aina ya mdumange, ili tujaribu kurudi nyumbani kwa watu wetu. Na ukiangalia wasanii wa kwanza waliofanya vizuri ni Q Chillah na TID.” 

“Kwahiyo tumefanya project kwa Abby Daddy, na Abby Daddy naye yupo kwenye mazungumzo na Diamond ilikuwa aingie kwenye hii ngoma. Tayari TID amemtumia ngoma kwa sababu ametoka kuchukua zile tuzo inabidi tumpongeze halafu tumpe kama wiki moja na nusu then tujue kama ataingia au vipi. Kwa sababu tunajua anaweza kuwa busy sana lakini ile ngoma tayari ni hit. Kwahiyo mwezi wa kumi na moja watu watapata vitu vizuri.”
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment