ROMA Ajisalimisha BASATA Kuwasikilizisha Wimbo Mpya Aliopanga Kuachia Kesho Siku ya Uchaguzi Oct.25

Roma Mkatoliki ameamua kuchukua jukumu la kwenda Baraza La Sanaa Tanzania, BASATA kuwasikilizisha wimbo wake mpya anaotarajia kuuachia Jumapili siku ya uchaguzi Oct.25 ili waupe baraka kuepuka kufungiwa.
Uamuzi huo umekuja kutokana na misukosuko aliyokutana nayo baada ya kutoa wimbo wake wa ‘Viva Roma Viva’ hivi karibuni, ambao BASATA waliufungia kutokana na madai kuwa hakuna ushahidi wa vitu vilivyoimbwa kwenye wimbo huo.
 Kupitia ukurasa wake wa Facebook Roma alipost ujumbe huu siku ya Jumamosi Oct.24;
“Kesho Ndiyo Ile Tarehe Niliyowaahidi
Kuwa Nitaachia ‪#‎KIBAO‬ Changu Kipya!!!!! /
Na Sasa Naelekea ‪#‎BASATA‬ Kuwasikilizisha Kabisa Kwanza!!! Wakitoa‪#‎GO_A_HEAD‬ Tu Basi Kesho Alfajiri ‪#‎KINANUKA‬ /
WAKIZINGUA NA MIMI NAWAZINGUA!!! /”
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment