Inakadiriwa kuwa asilimia 50 hadi 60 ya wanaume wenye maradhi ya kisukari wana tatizo la uume kushindwa kusimama. Watu wanaosumbuliwa na kiharusi na ulevi nao wana hatari kubwa sana kwa sababu ya uharibifu wa korodani Testicles kutokana na ulevi sugu na kupoteza Testerone. Pombe hupunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa manii (mbegu za kiume) na kupunguza madini ya zinki ambayo ni muhimu katika uzalishaji wa mbegu bora za kiume.
Watu wanaosumbuliwa na shinikizo la damu, magonjwa ya tezi, majeraha (kama vile kutokana na upasuaji wa viungo vya uzazi), matumizi ya dawa zenye kemikali bila mpangilio au ushauri wa wataalamu na maradhi ambayo hudhoofisha mtiririko wa damu kwenye uume. Hata hivyo, upungufu wa nguvu za kiume unatibika katika umri wa rika zote.

Usikose kufuatilia mada hii Alhamisi ijayo.

0 comments:
Post a Comment