MMH...CHIDINMA, TEKNO KUNA KITU KATI YAO!

Picha iliyowekwa na Chidinma Instagram.
SIKU chache zilizopita iliripotiwa kuwa staa anayekuja juu Nigeria aliyewahi kutoka kimapenzi na ‘video queen’ wa Kibongo, Agnes Gerald ‘Masogange’, Tekno yuko katika penzi jipya baada ya kuanikwa na mwanadada Chidinma.
Tekno ambaye anakimbiza na Ngoma ya Dulo ambayo kwa sasa ni gumzo nchini humo, juzi aliwekwa kwenye Ukurasa wa Instagram na mdada ambaye pia ni msanii, Chidinma aliyeisindikiza picha na ujumbe wa kimahaba.

Baada ya Chidinma ambaye amekuwa akitajwa kutoka na mastaa kibao Nigeria kuposti picha hiyo akiandika “Me and Bae”, Tekno alijibu mapigo kwa kuposti video inayowaonyesha wakiwa katika hali ya kimahaba, lakini Chidinma alipoulizwa na waandishi wa habari nini kiliendelea kati yao alikanusha kuwa na uhusiano na staa huyo mpya kwenye gemu la muziki Nigeria.
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment