Baada ya Kuonesha Kumkubali WIZKID, Alicia Keys Kumshirikisha Kwenye Wimbo Wake

Ayodeji Ibrahim Balogun, maarufu kama Wizkid ni msanii ambaye kwasasa wanamuziki wengi wakubwa wa Marekani, sio tu wanapenda muziki wake bali wanatamani kumshirikisha katika kazi zao.
Alicia n Wizkid
Akiwa Tanzania wiki iliyopita, Wizkid (25) aliwataja baadhi ya wasanii wakubwa duniani ambao wametaka kufanya naye kazi, kumshirikisha katika kazi zao.
Miongoni mwao alimtaja mfalme wa RnB, Robert Kelly ambaye alimpigia simu na kumtumia wimbo wake anaotaka arekodi naye, wimbo utakaokuwa kwenye album ya R.Kelly.
Msanii mwingine ambaye ameonesha kumkubali Wizkid ni Alicia Keys, ambaye amempa shavu la kutumbuiza kwenye hafla ya kampeni yake ya ‘Keep A Child Alive ‘ itakayofanyika Nov.5 jijini New York, Marekani. http://www.mwanalizombe.com/2015/11/baada-ya-kuonesha-kumkubali-wizkid.html Kwa mujibu wa mtangazaji wa East Africa Radio, Sam Misago ambaye alifanya naye mahojiano alipokuwa Dar, Wizkid amethibitisha kuwa baada ya hafla hiyo ataingia studio na Alicia Keys kurekodi wimbo ambao utakuwa ni wa Alicia Keys.

alicia wiz
Hit maker wa ‘No One’ ambaye ni mke wa producer Swiz Beatz, alianza kuonesha kupenda kazi za Wizkid miezi miwili iliyopita, kwa kupost video Instagram akicheza nyimbo zake ikiwemo ‘Ojuelegba’.
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment