KITUO CHA POLISI IKWIRIRI CHAVAMIWA NA MAJAMBAZI, ASKARI WAWILI WAUAWA

Mfano wa bunduki aina ya SMG zilizoibiwa.
Mfano wa bunduki aina ya SAR zilizoibiwa na majambazi.
Mfano wa bunduki aina ya Shotgun iliyoibiwa na majambazi.
Taarifa iliyoifikia leo asubuhi, inaeleza kuwa majambazi yamevamia kituo cha Polisi cha Ikwiriri, Rufiji mkoani Pwani na kuua Askari wawili na kupora silaha (bunduki) zilizokuwepo kituoni hapo.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo,huku askari wanaodaiwa kupotenza maisha ni Cop. Edgar aliyekatwa mapanga na Wp Judith aliyepigwa risasi ubavuni upande wa kulia na kutokea upande wa kushoto.

Hivi sasa hali ni tete katika eneo hilo na watu wamekusanyika huku polisi wakiongeza nguvu kusaka wauaji katika Tukio la uvamizi, kituo cha polisi Ikwiriri, Rufiji, Pwani.

Silaha zilizoporwa ni SMG 2, SAR 2, SHORTGUN 1, silaha 2 za mabom ya machozi na risasi 60 za smg.
Tutaendelea kujuzana kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia.

PATA HABARI HARAKA ZITUFIKIAPO. 
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA
KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO
TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142
-MICHUZI BLOG
Share on Google Plus

About Anonymous

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment