Imeamua kufanya hivyo kutokana na hali ya usafiri katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi cha Ubungo (UBT) kuwa mbaya hasa kwa abiria wanaokwenda katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Mwanza, Kagera na Kigoma kwa sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya kuongezeka.
Jana saa 12.20 asubuhi katika kituo hicho, abiria walikuwa ‘wakipambana’ kupata tiketi lakini karani wa Basi la Meridian Mustafa Mussa alisema hakuna aliyekuwa akiuziwa tiketi zaidi ya tatu. Baadhi ya wasafiri walilazimika kupanga foleni mara mbili ili kufikisha idadi ya tiketi walizohitaji.
“Sijui kwa nini wanatufanyia hivi, wanatulazimisha tukate tiketi tatu.. mimi nasafiri na familia yangu yote watu saba naambiwa nikate tiketi tatu hivi kweli inakuja?” alilalamika Joyce Munisi.
Ngenka Eliachim alisema kuna watu wanapanga foleni mara mbili, wanakata tiketi nyingi halafu wanaziuza.
“Wanatunyima haki sisi abiria, tumekuja tangu jana, tumelala hapa tunasubiri tiketi na tunaambiwa zimebaki za siku mbili,” alilalamika Eliachim.
Meneja Usalama Barabarani na Mazingira wa Sumatra, Geoffrey Silanda alisema wanatoa vibali kwa mabasi ambayo hayako kwenye ratiba ya kusafirisha abiria.
Matapeli kibao
“Nilikuwa nasafiri kwenda Mwanza ,nimefika hapa nikakosa tiketi, baadaye wakaja vijana wawili wakiwa na makaratasi, wakaniambia niwape Sh50,000 wanitafutie” alisema.
Alisema kutokana na shida aliyokuwa nayo aliwapa na matapeli hao walimwachia leseni ya gari kama dhamana lakini vyote vilibainika kuwa feki.

0 comments:
Post a Comment