Wakili wa Serikali, Diana Lukondo alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati kesi hiyo ilipotajwa. Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Huruma Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 13 mwakani itakapotajwa tena.
Mbali na Masamaki washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni vigogo wengine wa mamlaka hiyo, Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Wateja TRA, Habibu Mponezya, Meneja Udhibiti wa Forodha na Ufuatiliaji, Burton Mponezya, Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Biashara TRA, Hamisi Omary (48) na Haroun Mpande wa kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta TRA.
Washitakiwa saba wameachiwa kwa dhamana huku Mpande akiendelea kusota rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Masamaki, Habib Mponezya na Burton Mponezya wao waliachiwa huru kwa dhamana.
Wanadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi na Novemba 17, mwaka huu sehemu isiyofahamika, walikula njama za kuidanganya Serikali kuhusu Sh bilioni 12.7, kwa madai kuwa makontena 329 yaliyokuwa kwenye ICD ya Azam yametolewa baada ya kodi zote kufanyika, jambo ambalo si kweli.

0 comments:
Post a Comment