Tegete aliyeachwa na Yanga msimu uliopita kwa madai ya kushuka kwa kiwango, ameonyesha uwezo mzuri wa kufunga akiwa na Mwadui na kuacha maswali kuwa ilikuaje hadi akaachwa.
Straika huyo aliliambia Championi Jumamosi kuwa, makali yake ya ufungaji yasitafsiriwe vibaya kwani anachofanya ni kujituma na kufunga mabao kwa ajili ya timu yake na siyo ili aonekane yupo vizuri.
“Huwa nafurahi kila timu yangu inapofanya vizuri na namuomba Mungu atuongoze tufanikiwe kwani yeye ndiye kila kitu.”
Wakati huohuo, kocha wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ alisema Simba na Yanga zimekuwa zikiua vipaji vya wachezaji kwani ukiangalia kikosini kwake wachezaji wengi wametoka kwenye timu hizo na wanafanya vizuri.

0 comments:
Post a Comment